Breaking News, Home News, international News, Comprehensive, up-to-date News coverage, aggregated from sources all over the world...

Tuesday 11 June 2013

Jacob Zuma says 'all are praying' for Nelson Mandela


South African President Jacob Zuma says Nelson Mandela is "very serious but stabilised" in hospital and that "all are praying" for his recovery.
 
Mr Zuma said the doctors were doing a "very good job", adding that the former president was a "good fighter".
The 94-year-old is spending his fourth day in a Pretoria hospital suffering from a recurrent lung infection.
Relatives, including his ex-wife Winnie Madikizela-Mandela, visited the ailing former leader on Monday.
The former president has been in intensive care since he was admitted to the hospital on Saturday for the third time this year.
In December, Mr Mandela spent 18 days undergoing treatment for a lung infection and gallstones.
'Good fighter' Referring to Mr Mandela as "the father of democracy in South Africa", Mr Zuma said: "We need him to be with us and I'm sure all the messages that have been pouring in to wish him a speedy recovery are highly welcome.

Nelson Mandela in June 2010 


Turkey protesters defy PM's threats

Protesters by bonfire in Taksim Square, Istanbul, 11 June 2013
 
Clashes between Turkish protesters and police continue in Istanbul's Taksim Square, despite the PM's warning that he will not back down.

Police firing tear gas cleared the square on Tuesday morning, but protesters returned later in the day.

Istanbul's governor, Huseyin Avni Mutlu, said operations would go on night and day to clear the square.

Protests began 12 days ago over the redevelopment of nearby Gezi Park.

The protests then widened, with demonstrators accusing Mr Erdogan's government of becoming increasingly authoritarian and trying to impose conservative Islamic values on a secular state.

"We will continue our measures in an unremitting manner, whether day or night, until marginal elements are cleared and the square is open to the people," Mr Mutlu said in televised comments. 

Marekani yataja sababu nne za Obama kuja Tanzania



Marekani imetaja sababu nne ambazo zimemfanya Rais Barrack Obama kuijumuisha Tanzania katika ziara yake ya bara la Afrika.
Rais Obama amepanga kulitembelea bara la Afrika kuanzia Juni 26 hadi Julai 3, mwaka huu na atazitembelea pia Senegal na Afrika Kusini.

Kiongozi huyo wa Marekani ambaye baba yake mzazi ni mzaliwa wa Kenya, anatarajiwa kuwasili nchini Julai Mosi kwa ziara ya siku tatu. Atakuwa Rais wa tatu wa Marekani kuitembelea Tanzania baada ya Bill Clinton mwaka 2000 na George Bush mwaka 2008.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Balozi wa Marekani, Alfonso Lenhardt alisema sababu ya kwanza ya Obama kuja Tanzania ni kutokana na kuwa mfano wa utawala bora, demokrasia na ushirikishaji wa watu wake wakati wa kufanya uamuzi unaogusa maisha yao ya kila siku.

Alisema kuwa Tanzania ni nchi ya mfano linapokuja suala la uongozi bora na ndiyo maana imekuwa na amani na utulivu kwa muda mrefu ikilinganishwa na nchi nyingi za Kusini mwa Jangwa la Sahara.

“Nchi nyingi za Afrika zinazoizunguka Tanzania zimekuwa na matatizo ya vita vya wenyewe na hata ukosefu wa utawala bora,” alisema Balozi Lenhardt ingawa alidokeza kuwa katika siku za karibuni imekuwa ikikabiliwa na changamoto mbalimbali kutokana na matukio ya uvunjifu wa amani.

Balozi Lenhardt alisema sababu nyingine inayomfanya Rais Obama kuja Tanzania ni kutokana na jitihada za Serikali ya Marekani kutengeneza mazingira mazuri ya uwekezaji na kasi ya ukuaji wa uchumi.

“Rais Obama anakuja kuunga mkono juhudi za Watanzania katika kutengeneza mazuri ya uwekezaji lakini bila kusahau kuwa kasi ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania imeivutia Serikali ya Marekani,” alisema.

Balozi Lenhardt alitaja sababu nyingine inayomleta Rais Obama kuwa ni kuisaidia Tanzania kuendeleza fursa mbalimbali za kujiletea maendeleo.

Alisema uendelezaji huo wa fursa una lengo la kuisaidia Serikali ya Tanzania kukabiliana na tatizo la umaskini.

Alisema Marekani ni moja ya nchi zinazoongoza kwa kutoa fedha nyingi za misaada na akisema kwa mfano, mwaka 2012 pekee ilitoa Dola 750 milioni.

Aidha, alisema nchi yake imekuwa ikitoa misaada mingi kupitia Shirika la Millenium Challenge (MCC), ambayo imejikita zaidi katika kusaidia sekta za umeme, maji na miundombinu.

MWENYEKITI WA CCM DKT JAKAYA KIKWETE AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM KUPOKEA RASIMU YA KATIBA MPYA



Mwenyekiti wa CCM na Rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania, Dkt Jakaya Kikwete akiongoza kikao cha maalum ya CCM Kamati Kuu kilichokutana jana usiku mjini Dodoma kwa ajili ya kuipokea Rasimu ya Katiba mpya, iliyosomwa hivi karibuni.

Monday 10 June 2013

BREAKING NEWS: MSANII WA BONGO MOVIE AFARIKI DUNIA

                                          Marehemu Jaji Khamisi (Kashi)


Habari iliyotufikia hivi punde ni kwamba msanii wa filamu nchini Jaji Khamisi (Kashi)aliyewahi kutamba na michezo ya ITV enzi zile akiwa na wasanii kama mzee masinde,samson na wengine katika mchezo wa Tamu chungu na mingine mingi Amefariki dunia mchana huu katika hosptali ya taifa ya muhimbili alikokuwa amelazwa,akizungumza na the super stars tz raisi wa shirikisho la wasanii amesema kuwa tasnia yake bado inaendelea kukumbwa na majanga  lakini amedai yote ni kazi ya mungu. Nae mzee masinde ambaye alikuwa nae katika kundi moja akiwa kama kiongozi wake amesema kashi ni msanii ambaye alikuwa mpiganaji na kwa hakika ni pigo kubwa katika tasnia yetu Mungu ailaze roho ya marehemu Jaji Khamisi (Kashi)
mahali pema pepponi Amini.
 
 


 
 



Wednesday 5 June 2013

Absalom Kibanda, amerejea nchini kutoka Afrika Kusini alikokwenda kutibiwa

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda, amerejea nchini kutoka Afrika Kusini alikokwenda kutibiwa.
 
Kibanda ambaye pia ni Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya New Habari 2006 Limited, aliwasili nchini jana saa 7.55 mchana, akitokea Hospitali ya Milpark nchini humo, ambako alilazwa kwa miezi mitatu kisha kukaa hotelini kwa muda, baada ya kuvamiwa na watu wasiojulikana wakati akirejea nyumbani kwake, Mbezi Juu, jijini Dar es Salaam, Machi 5, mwaka huu. 

Kinana: Bora kuwa na wana-CCM wachache wazuri kuliko wengi walio hovyo


Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana, amesema ni bora chama hicho kuwa na wanachama wachache walio wazuri kuliko kuwa nao wengi walio hovyo.

Kiongozi huyo wa CCM, alitoa kauli hiyo wakati akifungua mkutano wa viongozi wa matawi na mashina wa chama hicho, uliofanyika kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea juzi.

Akitoa hotuba yake mbele ya mamia waliohudhuria mkutano huo, Kinana alisema si kwamba CCM ilikuwa imeshindwa katika kata sita mjini Songea katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, bali ni wana-CCM wenyewe ndio waliopoteza.

“Sio kwamba CCM ilikuwa imeshindwa kushika kata hizo bali ni baadhi ya wana-CCM ambao ni wabinafsi wenye kufikiri kuwa wengine hawawezi kuongoza isipokuwa wao ndio waliokabidhi kata hizo kwa wapinzani” alisema na kuongeza:

 “Safari hii katika Uchaguzi Mkuu ujao tutakuwa wakali, bora tuwe na wana-CCM wachache walio wazuri kuliko kuwa na wengi lakini wa hovyo. Tutajiandaa kwa chaguzi zijazo kwa kupeana madarasa.”

Alisema ni marufuku kwa watendaji wa chama hicho kuwa mawakala kwa watu wanaotaka kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama hicho.

Kinana aliahidi kufanya ziara rasmi katika mkoa wa Ruvuma mwezi ujao baada ya mwezi Mtukufu wa Ramadhan, aliuambia umati uliohudhuria kwamba, ili kusimamjia utekelezaji wa ahadi ambazo chama hicho kiliwahaidi Watanzania ili  mwaka 2015 kiwe na la kuwaambia wananchi.

Kinana akiwa mkoani humo kwa ziara ya siku moja alishiriki shughuli maalumu ya kuwakabidhi nishani ya mwenge wa uhuru wapiganaji uhuru wa Tanganyika kwa niaba ya Rais kabla ya kurejea jijini Dar es Salaam.