Breaking News, Home News, international News, Comprehensive, up-to-date News coverage, aggregated from sources all over the world...

Thursday 18 April 2013

MAHAKAMA NCHINI PAKISTANI INATOA AMRI YA KUKAMATWA ALIYEKUWA RAIS WA NCHI HIYO PERVEZ MUSHARRAF.....

 
 

A spokeswoman for Musharraf, Saima Ali ada, said his legal time was trying to decide the next move [AFP]
Mahakama kuu ktk mji wa Islamabad nchini Pakistan imeamrisha kukamatwa kwa aliyekua raisi wa zamani wa nchi hiyo kufuatia tatizo la kukwaruzana na mahakimu mwaka 2007.

Mahakama kuu ya nchi hiyo imeamua kutupilia mbali dhamana ya ndugu Musharraf na kuamrisha akamatwe. Washabiki wengi wa Musharraf walikusanyika nje ya mahakama huku wakipipiga kelele kwamba anachofanyiwa Musharraf sio uadilifu.
Mzungumzaji wa chama cha Musharraf All Pakistan Muslim League amenukuliwa akisema kwamba chama chake kitakata rufaa dhidi ya hukumu hiyo. Lakin kama itashindakana ana matumaini makubwa kwamba ndugu Musharraf atawekwa kizuwizini akiwa nyumbani (under house arrest).
Musharraf anashikiliwa kwa makosa matatu likiwemo la kuhusika na mauwaji ya Benazir Bhuto na mauwaji ya kiongozi mwengine wa kabila la Baluch yaliyotokea mwaka 2006 wakati akiwa Rais.
 



No comments:

Post a Comment