Breaking News, Home News, international News, Comprehensive, up-to-date News coverage, aggregated from sources all over the world...

Friday 29 March 2013

JENGO LA GHOROFA 16 LAPOROMOKA NA KUUA KATIKATI YA JIJI LA DAR ES SALAAM , TANZANIA.

Habari  NA  Neema Malley
Baadhi ya watu waliowahi kufika kujaribu kutoa msaada bila mafanikio hapa wakiwa wamekwama baada ya kukosa vifaa vya kutosha.

Waokoaji wakijitahidi kutumia mikono kuondoa kifusi hicho ili kuweza kuwaokoa watu waliofukiwa.
Hivi ndivyo hali ilivyokuwa
...Waokoaji
Juhudi zinaelekea kulala.
Moja kati ya magari yaliyokuwa eneo hilo likiwa limeangukiwa na mabaki ya jengo hilo.
(PICHA KWA HISANI YA SUFIANI MAFOTO, HABARI MSETO BLOG & AUDIFACE BLOG
 
 
 
 
 

MIILI ya watu wawili imepatikana na majeruhi 13

pamoja na magari manne kwenye eneo la kisutu mtaa wa

Indira Gandhi na Morogoro road ambapo jengo la

ghorofa 16 limeanguka na kusababisha hali ya

taharuki kwa wakazi wa eneo hilo .

Kwa mjibu wa bango lilikuwepo katika eneo

lilionyesha kuwa jengo hilo linamilikiwa na Shirika

la Nyumba NHC na Ladha Contruction ambalo lilikuwa

linajengwa na Luck Contruction ambapo lilisajiliwa

na Contructor Registration Board(CRB).

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam

Mkuu wa Mkoa Bw.Meck Sadik alisema tukio hilo saa

2:46 asubuhi ambapo linakadiriwa kuwa na watu zaidi

ya 60.

Bw.sadiki alisema anashindwa kuzungumzia chochote

kwa ufasaha kutokana kuwa bado mapema hivyo

aliwataka waandishi na wananchi kuwa na subira

wakati uokuaji unaendelea.

Mbali na hali hiyo pia kulisikika sauti za watu

kutoka chini ya kifusi wakiomba msaada wa kuokolewa

ndipo mmoja wa askari aliyekuwa ameshika kipaza

sauti aliwatuliza wahanga hao.

"Tulieni watanzania wenzenu wapo hapa kwa ajili ya

kuwaokoa poleni sana kwa uchungu mnaoupata mtatoka

mkiwa hai"alisema askari polisi.

Sambamba na hilo ingawa raia walionekana kuwa na

majonzi lakini walikuwa mstari wa mbele kuwasaidia

waokoaji kuhakikisha waliofunikwa na kifusi

wanaokolewa wakiwa salama.

Kabla ya hapo jeshi la polisi liliwazuia watu

wasishughulike na kitu chochote ila baadaye

wakaonekana kuhelemewa ndipo saa 5:17 wananchi

walilivamia eneo hilo na kuanza kuokoa.

Katika eneo la tukio zoezi la uokoaji lilionekana

kuwa zito kutokana hofu ya kuwafunika walio hai

ambao wamefunikwa na kifusi.

Majira ya Saa 6 Mchana Jeshi la Wananchi(JWTZ)

pamoja na Jeshi la kujenga Taifa(JKT) walionekana

katika eneo la tukio wakipanda juu ya kifusi la

jengo lililoanguka bila vitendea kazi ambapo baada

ya dakika chache walionekana kushuka hali

iliyoashilia  ni kutokana na kutojuwa nini la

kufanya.

Hivyo kutokana na ukosefu huo JWTZ pamoja na JKT

mpaka saa 7 mchana walijikuta wanaungana na wananchi

kupanga mstari mmoja ambapo walikuwa wanaokota

tofari moja moja wakiwa wanapasiana.

Mbali na hilo uhaba wa vitendea kazi lilikuwa ni

moja ya tatizo lililokwamisha zoezi hilo kwa kiasi

kikubwa pamoja na hofu ya kuwafukia waliochini

ambapo wapo hai.

Kwa upande mwingine Jeshi la zimamoto lilionekana

likimwaga maji kupunguza fumbi kwa waokoaji pamoja

na walio chini ya kifusi.

Huduma ya maji ilikuwa inatolewa bure ili kupunguza

kiu kwa waliokuwepo katika eneo la tukio pamoja na

hali ya ulinzi iliimarika kwani jeshi la kutuliza

fujo(FFU) walionekana na mbwa wa usalama .

Mpaka mchana viongozi mbalimbali waliudhuria katika

eneo la tukio akiwemo rais Kikwete,Mkuu wa Mkoa,Mkuu

wa Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam

Kamanda Suleiman Kova .

No comments:

Post a Comment